Diamond Platnumz - Upofu paroles de chanson

paroles de chanson Upofu - Diamond Platnumz



Mi kweli natamani siku iwezekane
Nifumbue macho mi kuona
Nijue sababu gani, unanipenda sana
Wakati siwezi mi kuona?
Mi kweli natamani siku iwezekane
Nifumbue macho mi kuona
Nijue sababu gani, unanipenda sana
Wakati siwezi mi kuona?
Mara nyingi peke yangu nawaza
Namuomba Mungu nisije kukwaza
Nikaja kukupa maudhi na nafsi kuichoma
Chei, tena usiku mzima nalia darling
Napiga goti kwa Mola nasali
Azidi tupe baraka tusije kosa dona
Eh, mi macho yangu nimejaliwa mboni lakini nuru sina
Ningekuwa na uwezo ningefanya kazi nikuhudumie
Upofu wangu ndo kikwazo kikubwa, mwenzako raha sina
Lakini unanijali, mbali na mengi unanipenda sana
Mi kweli natamani, siku iwezekane
Nifumbue macho mi kuona
Nijue sababu gani, unanipenda sana
Wakati siwezi mi kuona?
Mi kweli natamani siku iwezekane
Nifumbue macho mi kuona
Nijue sababu gani, unanipenda sana
Wakati siwezi mi kuona?
Nasikia kuna rangi ya upendo
Ili upendwe kuna pozi za mwendo
Utanashati, udambudambu na urembo mi sina
Mi natamani nitazame
Kwa ardhi na mbingu nilalame
Nipande mawingu na niiname
Uwenda nikaona
Eh, mi macho yangu nimejaliwa mboni lakini nuru sina
Ningekuwa na uwezo ningefanya kazi nikuhudumie
Upofu wangu ndo kikwazo kikubwa, mwenzako raha sina
Lakini unanijali, mbali na mengi unanipenda sana
Mi kweli natamani siku iwezekane
Nifumbue macho mi kuona
Nijue sababu gani, unanipenda sana
Wakati siwezi mi kuona?
Mi kweli natamani siku iwezekane
Nifumbue macho mi kuona
Nijue sababu gani, unanipenda sana
Wakati siwezi mi kuona?
Nikuone mama, niweze tazama
Every body say ee-eeh ee-eh ee
Ee-eh ee-eh ee, eh
Ee-eh ee-eh ee, I love you, nakupenda
Tena! Ee-eh ee-eh
Ee-eh ee-eh ee, eh
Ee-eh ee-eh ee, I love you, nakupenda
Say ee-eeh ee-eh ee
Ee-eh ee-eh ee, eh
Ee-eh ee-eh ee, I love you, nakupenda




Diamond Platnumz - Upofu
Album Upofu
date de sortie
12-12-2014

1 Upofu




Attention! N'hésitez pas à laisser des commentaires.