Ibraah - Nani текст песни

Текст песни Nani - Ibraah



Asubuhi kumekucha
Wingu limetanda
Na mvua yata kunyesha
Na uko mbali mama
Maji takitiririka
Oh baridi itanishika
We ndo chanda chema
Uhakika unanikatisha tamaa
Utaambiwa binadamu
Ah kila mmoja ana mapungufu yake
Sijui nilipoteleza mama
Si ungeniambia
Nimemiss tabasamu
Kutwa kucha
Picha kummezea mate
Yangu fimbo umeibeza
Ah katu hautaki kuitumia
Labda hesabu za kutoa
Mi niligawanya baby unisamehe
Na ile hasi nikafanya chanya
Baby unisamehe
Na hata emoji za kulia
Nazo kutumia nazo zikome
Japo nipate furaha
Ah huruma unionee
Maana hii hali, hata haifichiki
Kutwa wima cha mpingo, kisiki
Maana hata nikiona michezo ya njiwa
Ah huwa naitamani
Kama si wewe
Nitampenda nani?
Nitampenda nani?
Nitampenda nani
Nani nitampenda
Nitampenda nani?
Nitampenda nani?
Nitampenda nani
Nani nitampenda aah
Eh penzi usifanye kwa chombo cha usafiri
Ikawa umeshuka uje utanikatili
Nitakuwaga mental Niko dhahari
Si unasikia
Penzi la dhati daima la wawili
We fanya na urudi lisiwe batili
Ka wafanya kusudi ni ukatili
Mi naumia
We ndo yangu hifadhi
Labda nilikosea msimbo
Kweli kupenda kazi
Wangu umegeuka fimbo o
Mi ndo lako koroboi
Lile lisilo zima
Aha si ulisemaga hauchomoi
Kumbe imani ulinipima ah
Pia ulisema haudonoi
Wameiteka mazima
Ahaa simung'unyi sikohoi
Sina vyangu nimechina
Maana hii hali, hata haifichiki
Kutwa wima cha mpingo, kisiki
Maana hata nikiona michezo ya njiwa
Ah huwa naitamani
Kama si wewe
Nitampenda nani?
Nitampenda nani?
Nitampenda nani
Nani nitampenda
Nitampenda nani?
Nitampenda nani?
Nitampenda nani
Nani nitampenda aah



Авторы: Ibrahimu A N


Ibraah - Steps
Альбом Steps
дата релиза
08-05-2020




Внимание! Не стесняйтесь оставлять отзывы.