Kidum - Mapenzi paroles de chanson

paroles de chanson Mapenzi - Kidum



Uh uh uuh uuh, eeh
Mapenzi yo yo yo
Kama ni mapenzi
Ya kuniudhi kila saa
Ya kunifanya mi kulia
Na kama huridhiki
Na mbona hujasema
Ili niweze rekebisha
Nilidhani mambo shwari
Nikiamini u kwangu
Na kukusifu kwa wazazi
Hujali tena hisia zangu
Sijui tunapokwenda
Lakini najua tulipotoka
Kutoka sitoki nimetekwa nyara
Kukuwacha siwezi kibarua ngumu
Nashindwa ni nini nitafanya uridhike
Nimetekwa ndani
Mtandao wa mapenzi
Basi nakuomba
Uniteke tu bila mateso
Nimezama, nimezama
Ndani ya bahari, la penzi lako
Siwezi, kusonga mbele
Kurudi nyuma, sielewi
Haya mapenzi ya fujo hayafai
Kama unanipenda
Jaribu kunipa raha
Mi nashangaa
Watu wakisema
Eti tunapendana
Japo tunazozana
Ni vizuri mamii
Nyumba kuwa na siri
Lakini jaribu, tusuluhishe
Bila hivyo
Itakuwa mchezo, wa kuigiza
Kwenye mambo bandia
Mimi sitaki
Mambo ya kujifanya
Eti tunapendana
Tena tunatesana, uuuh
Nimejaribu sana kujitoa ndani (aah aah)
Kila nikipanga napangua mwenyewe (aah aah)
Natamani sana ungeelewa hivyo
Mimi mateka
Mimi pumbavu
Wa penzi lako
Nieleze ni lini ntakuwa huru
Tazama, nimezama (tazama yooh)
Ndani ya bahari, la penzi lako
Siwezi, kusonga mbele
Kurudi nyuma, sielewi
Haya mapenzi ya fujo hayafai
Kama unanipenda
Jaribu kunipa raha
Jaribu baby, uuh woo
Mambo, ya kunifanya kumbafu haifai
Mambo yo yo yo yo yo yo yo
Haifai
Jaribu baby
Tusuluhishe



Writer(s): Jean-pierre Nimbona


Kidum - Compilation




Attention! N'hésitez pas à laisser des commentaires.