Kassim Mganga - Tajiri Wa Mahaba текст песни

Текст песни Tajiri Wa Mahaba - Kassim Mganga



Unajionaje wewe na unanionaje
Mimi ndio tajiri wa mahaba karibu nikutunze×2
Nimefunga safari ya tanga mpaka mombasa
Nimefika tawakali nakutazama nakukosa
Wala sioni dalili simboni nakukosa
Naambiwa namba unayopiga mwenyewe kaja poswa
Na wala mi sijali na vyako visa visa
Aliekufunza ujeuri mwambie kwangu umefika
Unajionaje na mi unanionaje
Mimi ndio tayari wa mahaba karibu nikutunze ×2
Kwani binti unatakaje au na wewe nikuimbie
Kama waliokosa fadhila badae unikimbie
Sema binti unatakaje au pengine nisivutie
Unimiliki peke yako niweke basi nitulie
Penzi langu nikuonjeshe sitaki unijutie
Nikulishe nikuvike nikiondoka unililie
Unajionaje wewe na mi Unajionaje
Mimi ndio tayari wa mahaba karibu nikutunze ×2
Mimi ndio yulee tajiri
Mimi ndio yule tajiri eeeeh
Ni mola kaniumba tajiri wa mahaba na simai
Haupendezi kuwa mkatili wa mapenzi na kutojali basi nakuomba uje unisitiri uwe mlinzi wa hii hali ulidake chozi la pili lisije fika lile la awali
Nideke nisahau madhira niliojazwa na wa awali alieshindwa nipa chakula na kudiriki kunilaza chini
Unajionaje wewe na mi Unajionaje
Mi ndio yule tajiri karibu nikutunze
Mimi ndio yule mimi ndio yule tajiri toka maza bay
Mimi ndio yule tajiri mimi ndio tajiri tajir toka tanga



Авторы: Kassim Mganga


Kassim Mganga - Tajiri Wa Mahaba
Альбом Tajiri Wa Mahaba
дата релиза
08-10-2015




Внимание! Не стесняйтесь оставлять отзывы.